Breaking News

487 waitimu chuo cha ualimu ngazi ya Chet

Picha ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorius Luoga akiongea na wanachuo Chuo cha Ualimu TTC Tarime hawapo pichani katika mahafari ya 23.



CHUO cha ualimu TTC Tarime Mkoani Mara wananchuo 487 wameitimu mafunzo ya ualimu daraja la (111)A, katika mahafari hayo ya 23 mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorius Luoga.
 
Katika mahafari hao Mmoja wa wananchuo Devotha Mangarila akisoma risala alizitaja chanamoto zinazokumba chuo hicho huku wadau wote wa maendeleo kutoka  nje na ndani kujitokeza kwa wingi kutoa michango yao ili kusaidia na kuboresha miundo mbinu na wanachuo kupata mahali pazuri pa kujisomea.
 
Akisoma risala kwa mgeni rasimu mkuu wa wilaya Tarime Glorius Luoga mkuu wa chuo hicho Nicholaus Magige alisema kuwa  wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa maji,uchakavu wa majengo,ukosefu wa maabara,ukosefu wa maktaba,upungufu na uhaba wa nyumba za watumishi hali ambayo inasabisha kuwa na kilio cha mda mrefu bila msaada.
 
Aidha  Magige alisema kukubali kuwa mgeni rasimi wa maafali ya 23 ya chuo cha ualimu Tarime mkoani Mara utakuwa suluhisho la kilio cha mda mrefu ambacho kimekuwa kikitolewa na chuo hicho kwa kila mgeni ambaye anakuja kutembelea chuo hicho.
 
Sanjari na changamoto hizo Magige alisemakuwa chuo hicho wahitimu wa mwaka wa pili daraja la tatu A, walisasjiliwa 2013 wakiwa 503 ambapo wanaohitimu ni wanachuo 487 huku 16 hawakuhitimu kwasababu mbalimbali ikiwemo kihama na kifo.
 
Naye mkuu wa wilaya Tarime Luoga alisema kuwa atahakikisha wanaanda mkakati wa kuvuna maji hapo chuoni na kuondoa kero iliyopo ya maji kwanza huku kero zingine zilizobaki zikiendelea kutafutiwa uvumbuzi.
 
‘Nitahakikisha chuo kinakuwa na sehemu ya kuvunia maji na kupata maji ya uhakika na kupuinguza kero iliyiopo kama sio kumaliza kabisa’’alisema Luoga.
 
Aidha Luoga aliwataka wahitimu kuepuka kujiunga katika makundi ya wanasiasa badala yake watumiwe mda uliobaki kukamilisha kujisomea na kupanga mipango ya maisha kwa kuzingatia kuwa jamii na wazazi wanawategemea kufamnya vizuri  nawala sio kuwaangusha.
 
Hata hivyo mkuu wa wilaya amewaasa waanchua hao kuondokana na taamaa aza maisha pale wanapopata ajili
 
“Mkisha ajiliwa wengine munataka mafaniki ya haraka na kuelekea pasipositahili hebu jaribu kuepukana nahilo kwa lengo la kujiletea maendeleo” alisema Mkuu wa Wilaya.
 
Sanjari na hayo Mkuu wa wilwyw huyo aliongeza kuwa Serikali haina budi  kutoa ajira kwa waitimu hao ambao mwaka huu wameitimu Ngazi ya Cheti kwani kubadilika kwa mitahara kukmewakuta tayari wanaitimu hawa.
 
“Mimi kama mutumishi wa Serikali nashauri Wizara ya Elimu kuangalia jaira kwa wamnachuo walimal;iza ngazi ya Cheti ili badae wasaidiwe na kujiendeleza ili kufikia Sitashahada” alisema ,.

No comments