Breaking News

CHEKA UONGEZE SIKU ZA KUISHI 2

 Dada mmoja alikuwa bafuni akioga,mara akasikia hodi ikipigwa mlangoni,akajibu karibu huku akijisetiri kwa taulo na kanga ili akampokee mgeni.Alipofungua mlango,akakutana uso kwa uso na kijana mmoja kipofu aitwaye John,akamkaribisha kiti,kwa sababu anajua John ni kipofu,akavua taulo lake na ile khanga,akachukua mafuta ya lotion akaanza kujipaka kwa mbwembwe na pozi za kila aina.
"Enhee rafiki yangu john,nambie,kuna jipya?umeadimika saana rafiki yangu.John akamjibu,"yaap ni kweli niliadimika saana kwasababu nilikuwa China kufanyiwa operation ya macho na sasa nina uwezo wa kuona vizuri kabisa,kwa hiyo lengo la kuja hapa ni kukualika uje katika sherehe niliyoiandaa kujipongeza kwa operation kwenda vyema.

No comments